Serikali imewataka wananchi kuwapa ushirikiano watafiti wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu wanaozunguka katika maeneo mbalimbali nchini ili zipatikane tawimu sahihi zitakazoweza kutumika katika kufuatailia na kutathmini utekelezaji wa mipango na program za maendeleo katika ngazi ya taifa, kikanda na kimataifa.
Kauli hiyo ya serikali imekuja kufutia kuanza kwa tafiti mbili katika sekta ya kilimo, kiuchumi na kijamii katika mikoa yote ya TANZANIA Bara na ZANZIBAR zikilenga kubaini ufanisi wa program zilizopo na changamoto zinazowakabili wananchi katika sekta hizo
.Waafiti kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu wamesema tafiti hizo tayari zimeanza kufanyika kuanzia tarehe tano novema ikihusisha mikoa yote ya tanzania bara na visiwani ambapo jumla ya maeneo 1352, maeneo 1234 yapo Tanzania bara na maeneo 118 ni kutoka Zanzibar kwa kuzihusisha kaya 16224, 14808 kutoka Tanzania bara na 1416 kutoka Tanzania Zanziba
SUMA TEBELA, MENEJA WA NBS MKOA WA KIGOMA AKIWA NA ENDREW PUNJIRA, AFISA MASOKO WA NBS WAKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI KUELEZEA MAENDELEA TAFITI ZILIZO ANZA KUFANYIKA NOVEMBA TANO MWAKA HUU NA KUTARAJIWA KUDUMU KWA KIPINDI CHA MIEZI MIWILI KATIKA MAENEO MBALIMBALI NCHINI
Watafiti hao kutoka ofisi ya taifa takwimu wamesema tafiti hizo ni muhimu kwa manufaa ya umma ambapo tafiti za kiuchumi na kijamii zitahusisha majengo na shughuli zote za kiuchumi zilizopo ilihali tafiti za kilimo zitahusisha mashamba makubwa na madogo katika kilimo na ufugaji.
No comments:
Post a Comment