Monday 16 December 2013

Kigoma yaanza kutekeleza mpango wa “Matokeo Makubwa Sasa” katika Sekta ya Elimu




Picha ya majengo ya Utawala na Madarasa yatakavyokuwa baada ya ujenzi Kigoma Grand high School kukamilika
Pichan ya jengo ya Bwalo litakavyokuwa baada ya kukamilika ujenzi Kigoma Grand high School kukamilika
Eneo la majengo ya mabweni yatakavyokuwa baada ya ujenzi Kigoma Grand high School kukamilika

Kigoma yaanza kutekeleza mpango wa “Matokeo Makubwa Sasa” katika Sekta ya Elimu
Ili kuimarisha na kuboresha elimu ya Msingi na Sekondari mkoa umeweka mipango na mikakati mbalimbali kuhakikisha inatimiza adhima ya Serikali ya mpango wa Matokeo Makubwa sasa.
Katika kukabiliana na upungufu wa shule za kidato cha tano na sita  Mkoa umeanzisha mradi wa shule Kuu ya Mkoa itakayoitwa (Kigoma Grand High School) itakayogharimu jumla ya Tshs. 29 bilioni, fedha hizi zitatumika kujenga madarasa, maabara, nyumba za walimu, huduma za jamii (maji, umeme, afya), maktaba, bwalo samani, majengo ya utawala, uzio wa shule, viwanja vya michezo na miundombinu mingine. Mchakato wa kupata fedha kwa jili ya ujenzi ulikwishaanza, hadi sasa michango imefikia kiasi cha Tshs. 237,041, 700.00

Kigoma Grand Kigh School inatarajiwa kuwa na michepuo ya masomo ya Sayansi 9 na Sanaa 5 ambapo itakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi kuanzia 1120 wasichana na wavulana.
Mkoa umedhamiria kuongeza ufaulu wa mitihani ya Taifa ya darasa la saba kutoka 31% na Mitihani ya Kidato cha nne kutoka 43% kufikia 60% mwaka 2013. Aidha katika  kuinua ufaulu mafunzo ya ziada kwa walimu wa shule za msingi wanaofundisha masomo ya Sayansi na Hisabati kutoka shule 206 hadi sasa yametolewa kwa walimu 412, hata hivyo mpango huu unategemewa kufanyika hadi ngazi ya walimu wa shule za sekondari.
 
Mipango mingine ni pamoja na kuongeza idadi ya uandikishaji wanafunzi wa awali na darasa la I, Kuhakikisha kuwa wanafunzi wa darasa la II wanajua KKK Kusoma, Kuandika na Kuhesabu kabla ya kuingia darasa la III, Mkoa unashirikisha wazazi na wadau wa elimu katika ujenzi wa miundombinu inayopungua katika shule zilizo katika kila halmashauri.

Mkoa unaishukuru serikali ya awamu ya nne kwakuupa Mkoa wa Kigoma kipaumbele wa kipekee na wa makusudi kabisa hasa katika kuimarisha miundombinu ya barabara kama ile ya Kidahwe – Nyakanazi; Kasulu – Uvinza – Katavi na Kidahwe – Ilunde – Tabora. Hali hii itavutia watu wengi kuja na hasa wafanyakazi wa sekta mbalimbali kufanya kazi katika Mkoa huu tofauti na hapo awali hivyo itachochea maendeleo na kuvutia wawekezaji na uwekezaji ndani ya mkoa wetu wa Kigoma.

1 comment:

  1. Safi sana, ila mpango usiishie kwenye makaratasi tu.

    ReplyDelete