Tuesday 11 April 2017

Matumizi ya Simbomilia (Barcordes) katika bidhaa ni jambo lisilokwepeka Kuelekea Nchi ya Viwanda Tanzania

Matumizi ya Simbomilia (Barcordes) au alama za utambuzi wa bidhaa katika masoko ni jambo lisilokwepeka kwa sasa ambapo Tanzania inaelelekea kweye nchi ya uchumi wa kati na viwada. 

Haya yameelezwa na Mkurugezi wa Taasisi ya Global Standard one (GS1) Tanzania Bi. Fatma Kange Salehe wakati wa kutia saini ya makubaliano na Halmashauri nane za Mkoa wa Kigoma.

Mkataba wa Makubaliano na Taasisi ya GS1 Tanzania unalenga kuwapa mafunzo na kuwajengea uwezo wajasiriamali katika Halmashauri ili waweze kutambua umuhimu wa kuwa na alama za utambuzi wa bidhaa katika masoko wanazozizalisha.

Mafunzo hayo yanatarajiwa kuzijumuisha Taasisi mbalimbali zitakazoshiriki katika utoaji wa mafuzo hayo kwa wajasiriamali kama vile Wakala la Vipimo, Mamlaka ya Mapato Tazania, Shirika la Viwago Tanzania, BRELLA, SIDO, TANTRADE.

Matarajio baada ya mafunzo haya ni, kuongezeka kwa mapato ndani ya Halmashauri, bidhaa nyingi kuwa katika soko rasmi kitaifa na kimataifa, kuongeza mnyororo wa thamani ya bidhaa zinazozalishwa na wajasiriamali, kuongezeka kwa wajasiliamali katika Halmashauri na, kuwanyanyua kiuchumi wajasiliamali wadogo.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Brigedia Jenerali Emanuel Maganga (mst) ambaye alishuhudia utiwaji wa makubaliano hayo kati ya GS1 Tanzania na Halmashauri za Mkoa wa Kigoma alisema kuwa lengo la Serikali ya Mkoa wa Kigoma ni kuhakikisha kwamba fursa zote za kilimo, uvuvi na madini zinafanyiwa kazi kisasa zaidi ili wananchi waweze kumiliki Uchumi. “ili wananchi wetu waweze kunufaika na kilimo, vuvi, madini  lazima kuwepo na mbinu sahihi za kuongeza thamani kwenye bidhaa zao wanazozalisha na zikubalike katika masoko ya ndani nje” alisisitiza.

“Ninaamini makubaliano haya yatakuwa na matokeo chanya ambayo yatawezesha bidhaa nyingi za Tanzania hususani wananchi wa Kigoma kuingia katika Masoko ya ndani na nje ya nchi hivyo kuinua pato la mtu mmoja mmoja na hatimae taifa zima” aliongeza Maganga.

Aidha, amewaasa watanzania kuanza kutumia Simbomilia (barcordes) za Tanzania badala ya kutumia za nje ya nchi. Alisisitiza kuwa kutumia simbomilia za Tanzania kutapunguza matumizi ya fedha za kigeni ambazo zingetumika kulipia uduma hiyo, pia itasaidia kutoa takwimu rasmi za wazalishaji wa Kitanzania, kwani unapotumia simbomilia za nje ya nchi bidhaa huonekana imetoka nchi nyingine na siyo Tanzania hata kama imezalishwa hapa nchini.

Kutokana na umuhimu wa jambo hili Maganga amewaagiza Wakurugenzi kuanza mafunzo haya kwa wajasiliamali ndani ya Miezi miwii tangu kutiwa saini ya Makubaliano na Taasisi ya GS1 Tanzania.

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Brigedia Jenerali Emanuel Maganga (katikati), Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma Bw. Charles Pallangyo (kulia) na Mkurugenzi wa GS1 Tanzania Bi Fatma Kange Salehe wakishuhudia utiaji wa saini kati ya Tasisi hiyo na Halmashauri ya Kakonko.

No comments:

Post a Comment