Monday 15 January 2018

ZAIDI YA ASILIMIA 85 KUANZA KIDATO CHA KWANZA JANUARI 2018 MKOANI KIGOMA

Zaidi ya watoto 16,448 sawa na asilimia 67.1  waliofaulu katika mtihani wa Taifa wa Darasa la saba 2017 Mkoani Kigoma wataanza masomo ya kidato cha kwanza mapema Januari 2018 ikiwa ni wale waliochaguliwa kwa awamu ya kwanza.
Haya yametolewa na Afisa Elimu wa Mkoa wa Kigoma Bw. Juma Kaponda katika kikao cha kutangaza matokea ya mtihani wa Darasa la saba Mkoani Kigoma kilichofanyika mwishoni mwa mwaka 2017.
Jumla ya watahiniwa 36326  wasichana 18746  na wavulana 17580 ambao ni sawa na aslimia  99.25 ya wanafunzi walifanya mtihani wa kuhitimmu darasa la saba Mkoani Kigoma mwaka 2017, ambapo kati yao waliofaulu kwa alama za kuendelea na kidato cha kwanza ni 24,528 Wasicha 11,104 na wavulana 13,424.
Aidha wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2018 ni 16,448 sawa na aslimia 67.1 ya waliofaulu, hata hivyo wanafunzi 8080 sawa na asilimia 32.9 wamebaki bila kupangiwa shule wakisubiri hatua ya uchaguzi wa awamu ya pili.

 Mkoa umejiwekea mikakatai mbalimbali ikiwemo kukamilisha vyumba vya madarasa, ili kuhakikisha wanafunzi wote waliofaulu wanaweza kuanza masomo mapema kabla ya Februari. Mkoa wa Kigoma umeshika nafasi ya 18 Kitaifa katika ufaulu wa Mtihani wa darasa la saba.

No comments:

Post a Comment