Kongamano lina lengo la kuwakutanisha wafanyabiashara wa Mkoa wa Kigoma
na Tanzania kwa ujumla na wafanyabiashara wa nchi jirani za Burundi, DRC Kongo,
Zambia, na Rwanda ili kwa pamoja kujadili na kuafiki namna ya kukuza biashara
na uwekezaji kutokana na fursa zilizopo ndani ya nchi hizi hususan kwenye sekta
za viwanda, kilimo, mifugo, uvuvi, usafirishaji na biashara kwa ujumla. Kongamano
hili litaleta manufaa mengi kwa Mkoa,Washiriki na Nchi kwa ujumla ikiwemo:-
1. Kutangaza fursa za biashara na uwekezaji baina ya
nchi majirani
2. Kuwakutanisha wafanyabiashara/wawekezaji wa nchi
washiriki ili kubainisha fursa mbalimbali za kibiashara na uwekezaji
zitakazowezesha kuanzisha na kuendeleza miradi katika sekta za viwanda, kilimo,
mifugo, uvuvi, usafirishaji, na biashara kwa ujumla.
3. Kuanzisha mahusiano ya kibiashara na muingiliano
wa kibiashara baina ya nchi za Maziwa makuu za Tanzania, Burundi, Rwanda,
Zambia na Demekrasia ya Kongo.
4. Kuimarisha biashara za mipakani
5. Kujenga mazingira mazuri ya biashara na uwekezaji
baina ya nchi majirani
6. Kujenga muingiliano wa wajasiriamali na wawekezaji
au wafanyabiashara wakubwaa
7. Kujenga
moyo na tabia za ujasiriamali miongoni mwa vijana na wanawake wa mkoa wa
Kigoma
8. Kujenga mahusiano ya kudumu baina ya taasisi za
serikali,na sekta binafsi miongoni mwa nchi wanachama
Watanzania kutoka Mikoa yote wanaalikwa kuchangamkia fursa hii kwa
kushiriki kongamano ili kunufaika na fursa mbalimbali zitakazojitokeza ikiwa ni
pamoja na kunadi fursa za uwekezaji na biashara za mipakani, kujifunza mbinu
mpya za biashara na uwekezaji kutoka kwa washiriki sambamba na kutafuta wabia,
masoko, mitaji na teknolojia mpya.
Kongamano linatarajiwa kuwa na washiriki zaidi ya 300 na litaambatana
na maonesho (Exhibition) ya bidhaa na huduma mbalimbali kutoka Tanzania,
Burundi; DRC Kongo, Rwanda na Zambia.
No comments:
Post a Comment