Mkuu
wa Mkoa wa Kigoma Brig. Gen. (Mst.) Emmanuel Maganga leo amekutana na Bw.
Vincent Rico Mkuu wa Mradi wa Madaktari wasio na Mipaka na kuzungumzia namna ya
kuendelea kuboresha huduma za Afya Mkoani Kigoma.
Bw.
Rico ameeleza kuwa Medical Sans Frontiers (MSF) wataendelea kutoa misaada
mbalimbali katika sekta ya afya ikiwemo kusaidia kupambana na Malari, kuangalia
namna ya kusaida madawa pamoja na vitendea kazi katia Hospitali na vituo vya
Afya Mkoani Kigoma.
Kwa
upande wake Mkuu wa Mkoa wa Kigoma ametoa shukrani kwa MSF kwa juhudi zao kubwa
katika kuusaidia Mkoa wa Kigoma kwenyemasuala ya sekata ya Afya, amesisitiza
kuwa Mkoa wa Kigoma utaendelea kutoa ushirikiano wakati wote ili kuhakikisha
wananchi wa Mkoa wa Kigoma wanapata huduma bora za afya.
No comments:
Post a Comment