Wafanyabiashara
watakiwa kutojihusha katika rushwa kama njia ya kukwepa kuipa kodi
| Dkt. Ndunguru akisisitiza jambo katika kikao cha wafanyabiashara na Uongozi wa Mkoa wa Kigoma kilichofanyika jana katika Ukumbi wa Ofisi ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma |
Dkt.
Ndunguru ameyasema hayo wakati wa kikao maalumu alichokiitisha kati yake na
wafanyabiahsra pamoja na uongozi wa Mamlaka ya Mapato Mkoa wa Kigoama kufuatia
malalamiko na mgogoro wa baadhi ya wafanyabiashara kufungiwa maduka yao baada
ya kugomea utaratibu wa Matumizi ya mashine za kuuzia za kielektroniki EFD (Electronic
Fiscal Divices) uliowekwa na Serikali.
Akizungumza
na wafanyabiashara Dkt. Ndunguru alielezwa kuwa baadhi ya maaofisa kutoka Ofisi
ya Mamlaka ya Mapato mkoani Kigoma wamekuwa wakiwafuata wafanyabiashara na
kuwaomba fedha kidogo ili wawapunguzie makadirio ya kodi jambo ambalo
limelesababisha migogoro na chuki kati ya Ofisi ya Mamlaka ya Mapato Mkoa wa
Kigoama.
Aidha Dkt. Ndunguru amemwagiza Meneja wa Mamlaka ya Mapato Mkoa wa Kigoma afuatilie watumishi wanaosemekana kujihusisha na unyanyasaji wa wafanyabiashara na wale wasiozingatia maadili ya utumishi wa umma waweze kupewa onyo kali.
" Ofisi ya Meneja wa Mamlaka ya Mapato Mkoa wa Kigoma inatakiwa ifanye mikutano na wfanyabiashara au uongozi wa wafanyabiashara ili kupeana habari mbalimbai kwni migogoro mingine inatokana na kutokuwa na taarifa sahaii" aliongeza Dkt. Ndunguru.
Habari na Picha -G.D. Ng'honoli (Afisa Habari wa RS Kigoma)

No comments:
Post a Comment