Tuesday 18 March 2014

Mkoa wa Kigoma Wazindua Kampeni ya Lishe

Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma Eng. Dkt. John S. Ndunguru akitoa hotuba kwa wananchi wilayani Uvinza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya lishe Kimkoa.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma Eng. Dkt. John Ndunguru Mkuu wa Wilaya ya Uvinza Mwalimu Hadijah Nyembo wakifurahia burudani kutoka kikundi cha Mapigo Tisa (hakipo pichani) siku ya Uzinduzi wa kampeni ya Lishe.

Baadhi ya Maafisa na Watendaji wa ngazi mbalimbali katika Mkoa na Halmashauri wakifuatilia Hotuba aliyoitoa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma Eng. Dkt. John Ndunguru (Hayupo pichani) wakati wa kuzindua kampeni ya Lishe.

Eng. Dkt. John Ndunguru abaye ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma akitoa matone ya Vitamini A kama shughuli mojawapo ya kampeni ya lishe.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma Bw. Hamis Betese akishiriki kucheza ngoma ya asiliiliyoutumbuizwa na kikundi cha Mapigo Tisa.



Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigom Eng.  Dkt. John Ndunguru, na Mkuu wa Wilaya ya Uvinza Mwl. Hadijah Nyembo wakipata maelezo kutoka kwa mtaalamu wa Lishe walipotembelea banda la maonesho ya vyakula siku ya uzinduzi wa kampeni ya lishe.





Mkoa wa Kigoma umezindua rasmi leo kampeni ya lishe ki-Mkoa Kufuatia agizo la Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete alilolitoa siku ya Uzinduzi wa kampeni  ya lishe kitaifa Mwezi mei, 2013, kwamba kila Mkoa ufanye uzinduzi wa kampeni hiyo.

Akiwahutubia wananchi Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma Mhandisi Dkt. John Ndunguru kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa ameziagiza Halmashauri ziwe na mpango wa lishe wenye kutoa matokeo chanya kwa muda mfupi  kwa kutumia Rasilimali zinazopatikana Mkoani Kigoma.

Bado Serikali inaendelea kukabiliana na changamoto ya uelewa mdogo wa wananchi kuhusu masuala ya lishe katika jamii, kuanzia ngazi ya familia hadi kwa watendaji; ametaja baadhi ya visababishi vya utapiamlo ni ulaji duni na mbaya, maradhi mbalimbali, kutokuwa na uhakika wa chakula matunzo duni ya mama na mtoto, mazingira machafu, umaskini wa kipato na baadhi ya sera zisizotambua umuhimu wa lishe kwa maendelo ya nchi yetu.



Aidha ametoa wito kwa kwa wasanii, waandishi wa habari kutumia nafasi walizonazo katika kuielimisha jamii juu ya lishe ili kuisaidia Serikali kuboresha lishe kwa wananchi, elimu ya lishe izingatie uzalishaji na ulaji wa vyakula mchanganyiko.

Dkt. Ndunguru amesema kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi nyingi za Afrika kwa kuwa na kiwango kikubwa cha utapiamlo unaohatarisha ustawi wa watoto, mama wajawazito na maendeleo ya kiuchumi na Kijamii kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment