Thursday 17 April 2014

Balozi wa Ujerumani Nchini Tanzania awasili Mkoani Kigoma kwa ziara Maalumu.




Balozi wa Ujerumani Nchini Tanzania awasili Mkoani Kigoma kwa ziara Maalumu.
Uzalishaji wa asali na nta Mkoani Kigoma umeongezeka kutoka tani 100 za asali na tani 5 za nta mwaka 2007 hadi kufikia tani 346 za asali na 10 za nta mwaka 2013, ongezeko hili limesaidia kuinua kiwango cha mauzo ya wafugaji nyuki kutoka Shs. 315 milioni mwaka 2007 hadi  Shs. 2.14 bilioni mwaka  2013. 
      Balozi wa Ubelgiji nchini Tanzania Adam Koenraad akigawa kadi za Mawasiliano binafsi kwa wenyeji wake mara baada ya kuwasili jana katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma
 
Mafanikio haya yanatokana na juhudi zinazofanywa na Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Serikali ya Ubelgiji ambapo mradi wa kuendeleza ufugaji Nyuki umeboresha uchakataji,  na kutafuta masoko ya asali, nta na mazao mengine ya nyuki katika Wilaya za Kibondo na Kigoma ambapo jumla ya Shilingi Bilioni Moja na Milioni Mia saba (1,700,000,000/=) zilitolewa na Serikali ya Ubelgiji kusaidia mradi huo.
      Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kanali (mst.) Issa Machibya akitoa hotuba ya ukaribisho wakati Balozi wa Ubelgiji Nchini Tanzania alipotembelea Ofisini kwake jana asubuhi.

     Katibu Tawala wa Mkoa Mhandisi Dkt. John Ndunguru wa kwanza kushoto na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Lt. Col. (mst.) Issa Machibya wa pili toka kushoto pamoja na Balozi wa Ubelgiji nchini Tanzania wakisikiliza taarifa ya Mkoa ikitolewa na Katibu Tawala Msaidizi Sekshneni ya Mipango na Uratibu Bw. Georges Bussungu akitoa maelezo ya jumla kuhusu Mkoa wa Kigoma wakati wa ziara ya Balozi wa Ubelgiji ambaye yupo Mkoani Kigoma kwa ziara fupi ya kikazi.

Katibu Tawala Msaidizi Sekshneni ya Mipango na Uratibu Bw. Georges Bussungu akitoa maelezo ya jumla kuhusu Mkoa wa Kigoma wakati wa ziara ya Balozi wa Ubelgiji ambaye yupo Mkoani Kigoma kwa ziara fupi ya kikazi

     Balozi wa Ubelgiji nchini Tanzania Bw. Adam Koenraad akielezea namna nchi yake inavyopanga kushirikiana na Tanzania hususan Mkoa wa Kigoma katika masuala mbalimbali ya maendeleo kwa wananchi.

Viongozi mbalimbali katika Sekretariati ya Mkoa wa Kigoma wakiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Ubelgiji nchini Tanzania watatu kutoka kushoto

No comments:

Post a Comment