Monday 9 June 2014

Miundo Mbinu ya Kisasa kuufanya Mkoa wa Kigoma Kitovu cha Kibiashara kwa nchi za Burundi na Congo DRC



Miundo Mbinu ya Kisasa kuufanya Mkoa wa Kigoma Kitovu cha Kibiashara kwa nchi za Burundi na Congo DRC.

Uchumi wa taifa lolote duniani hutegemea ubora wa miundominu iliyopo katika sekta mbalimba inanazowezesha biashara na uwekezaji, miundombinu bora na ya kisasa inahitajika katika nchi yetu ili kuweza kushawishi uwekezaji wa ndani na nje mathalani uwepo wa Barabara, viwanja vya Ndege, bandari na nishati ya umeme. 

Eneo la maegesho ya meli katika Bandari Mkoani Kigoma eneo hili hupokea meli za mizigo na abiria kutoka nchi za Burundi , Kongo na Zaire.


Jenereta za kisasa za kuzalisha Umeme  mjini Kigoma.


Hayawi hayawi sasa yamekuwa ni msemo wa enzi na enzi wenye kuamsha shauku ya kile kilichongojewa kutimia, ndivyo ilivyo kwa wananchi wa Mkoa wa Kigoma ambao kila mmoja bila kujali itikadi aliyonayo kisiasa anakiri wazi tena hadharani nguvu na kasi ya kimaendeleo inayofanywa na Serikali ya awamu ya nne chini ya Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete kubadili sura ya Mkoa  na kuondoa  habari za kihistoria za ubovu wa Miundombinu ya Mkoa huu.

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Luteni Kanali (mst) Issa Salehe Machibya anathibitisha  kwa kusema miundo mbinu katika Mkoa wa Kigoma imeimarika kwa zaidi ya asilimia 85. 
Uwanja wa ndege Mkoani Kigoma baada ya kufaanyiwa maboresho na upanuzi.

Uwanja wa ndege Mkoani Kigoma kabla ya kufanyiwa upanuzi na maboresho.

Hapo nyuma tangu uhuru Mkoa wa Kigoma kwa upembeni wake katika sura ya Tanzania ulikuwa nyuma katika suala zima la maendeleo kwa kukosa kabisa Miundombinu bora kama vile Barabara, bandari, usafiri wa anga, miundo mbinu hii si kwama haikuwepo bali ilikuwepo lakini iliuwa na kiwango duni kiasi cha kutowezesha mawasilano na usafiri wa haraka kirahisi kwenda Mikoa mingine.

Ni dhahiri kabisa kuwa usumbufu huo sasa unaelekea  kukoma na kutokomea mara baada ya serikali ya awamu ya nne kugeuzia jicho lake katika Mkoa wa Kigoma, ambapo zaidi ya kilomita 200 za Barabara zimejengwa kwa kiwango cha lami Barabara zilizizokuwa na usumbufu kama vile  Mwandiga – Manyovu (kilomita 60); Kigoma – Kidahwe (kilomita 35.7) na Kidahwe – Uvinza (kilomita 76.6).


Ujenzi wa Barabara ya rami Kidahwe – Uvinza (kilomita 76.6) inayounganisha Mkoa wa Tabaora na Kigoma.


 Aidha ujenzi wa daraja la Kikwete katika mto Malagarasi lenye urefu wa mita 275 pamoja na kuinua tuta la bonde la mto Malagarasi lenye urefu wa kilomita 2 umekamilika, Ujenzi wa daraja hilo unaambatana na ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami pande zote mbili za daraja (approach roads) zenye urefu wa kilomita 48. Kufungua kwa daraja hili kutaunganisha Mkoa wa Kigoma na Mkoa jirani wa Tabora ambayo ndiyo njia kuu katika kuunganisha na Mikoa mingine Tanzania.

Mhe. Machibya anaeleza moja ya faida za kukamilika kwa daraja la Mto Malagarasi alimaarufu Daraja la Kikwete kuwa litatoa wigo mkubwa kwa Mkoa wa Kigoma kuwasiliana na mikoa mingie kiurahisi, wafanyabiashara wa mazao ya kilimo kama vile miwa, nanasi, ndizi sasa wanauwezo wa kusafirisha mazo hayo kwenda mikoa jirani ya Tabora na kwingineko kwa uharaka na muda wote wa misimu bila kukwama.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma (wa pili toka kushoto) Eng. Dkt. John S. Ndunguru akikagua moja ya Shughuli za ujenzi wa Barabara Mkoani Kigoma


Daraja la Kikwete katika mto Malagarasi lenye urefu wa mita 275 ambalo limekamilika.


Daraja la Kikwete katika mto Malagarasi lenye urefu wa mita 275 ambalo limekamilika.


Maeneo mengine ya miundombinu kama vile ya Reli, Bandari na Uwanja wa Ndege navyo havijasahaulika. Kwa mfano, Uwanja wa Ndege wa Kigoma, ambao umefanyiwa upanuzi kutoka mita 30 hadi 45 za sasa ili kuwezesha Ndege kubwa za abiria na mizigo kutua mkoani Kigoma.

Naye Mhandisi Dkt. John S. Ndunguru ambaye ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma kwa shauku anelezea namna Mkoa wa Kigoma unavyojipanga katika kutumia fursa ya Nchi jirani za Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambazo kwa kiwango kikubwa zinategemea sana upitishaji wa mizigo yake kupitia Tanzania Mkoani Kigoma. Aidha wasafiri watakaotumia Uwanja wa Ndege wa Kigoma kutoka nchi hizo wataongezea maradufu. Kukamilika kwa miundo mbinu hii ni ishara wazi kuwa Mkoa wa Kigoma unafunguka na kuwa kitovu cha kibiashara.

Baadhi ya wakazi wa Mkoa wa Kigoma wamekuwa wakikiri wazi kuwa Kigoma ya sasa si yazamani ambapo reli ya kati ndiyo pekee ilitegemewa kwa usafiri na usafirishaji, imani yao kwa sasa ni kwamba Miundombinu iliyowekwa sasa imeufungua mkoa wa Kigoma na fursa nyingi zimeanza kuonekana katika sekta ya kilimo na mifugo, Uvuvi, utalii pamoja na uwekezaji katika eneo Maalumu la Kigoma “Kigoma Special Economic Zone”.



Shughuli za Uvivi hufanywa na wakazi wa Kigoma katika Ziwa Tanganyika ambapo samaki na dagaa husafirishwa kwa wingi kwenda nchi jirani za Kongo na Burundi


Shughuli za Uvivi hufanywa na wakazi wa Kigoma katika Ziwa Tanganyika ambapo samaki na dagaa husafirishwa kwa wingi kwenda nchi jirani za Kongo na Burundi



Mhandisi Dkt. Ndunguru anafafanua kuwa jambo ambalo kwa sasa wanaihiaji wanakigoma sambamba na kuendelea kukamilishwa kwa mawasiliano ya Barabara, na Uwanja wa Ndege, kiu kubwa iliyopo mbeleni ni kukamilishwa kwa masoko ya mpakani katika maeneo ya Muyama (Wilayni Buhigwe) Mkarazi(Wilayani Kibondo) na Kagunga( Wilayani Kigoma) mwambao wa ziwa Tanganyika ambako soko la Kimataifa linajengwa.

Zipo biashara zisizo rasmi zinazofanywa na wanchi wa Tanzania na Burundi hasa waishio mpakani ambazo kimsingi hazina tija katika kukuza uchumi hivyo kujengwa kwa miundombinu ya masoko, vivuko vya madaraja, barabara na miundombinu ya huduma za kijamii kutawezesha kutoka katika biashara za kijadi kwenda katika biashara ya kimataifa na hivyo kukuza uchumi na kipato cha wananchi wa Mkoa wa Kigoma.

Soko la Kimataifa lililopo Wilayani Buhigwe katika Kijiji cha Nyamgali


Mahindi yaliyo hifadhiwa kienyeji Wilayani Kakonko Mkoani Kigoma, Mkoa wa Kigoma upo katika orodha ya Mikoa ya uzalishaji hapa Tanzani.


Bidhaa mbalmbali zitokanazo mazao ya nyuki Mkoani Kigoma, mbali na kuuza asali wananchi hutengeneza bidhaa kama mishumaa na kuongeza kipato.


Soka la Kimataifa lililopo Wilayani Buhigwe katika Kijiji cha Nyamgali


Mazao kama vile muhogo, karanga, ulezi inasemekana ndiyo chakula kitumiwacho na wakazi wa Burundi na kongo, mkoa wa Kigoma unazalisha mazao ya aina zote kwa hakika masoko ya mazo haitakuwa shida tukiwa na Miundombinu ya uhakika.

Aidha ujenzi wa bandari kavu katika eneo la Katosho Manispaa ya Kigoma/Ujiji ni faraja kubwa kwa wafanyabishara kutoka nchini Burundi ambao wamekuwa wakitoa maombi yao kwa uongozi wa Mkoa waruhusiwe kupitisha mizigo yao kupitia Barabara ya Dar es Salaam  Nyakanazi- Kibondo- Kasulu  kutoka bandari ya Dar es Salaam, badala ya  Dar es salamm-Nyakanazi- Rusahunga ambayo ni ndefu na ni gharama kubwa kwao.

Kwa hakika Miundombinu hususan ya Mawasiliano katika Mkoa wa Kigoma imeimarika, jitihada na nguvu ya Serikali zinaonekana wazi kwa wananchi, waswahili husema “ndondondo si chururu” miaka michache mambo yote yatakamilika kwani hatani mji wa Roma haukujengwa kwa siku moja.
Habari zote na Picha- Afisa Habari wa RS Kigoma

No comments:

Post a Comment