Saturday 3 December 2016

Watumishi Mkoani Kigoma Wahimizwa Kufanya Mazoezi ya Mwili kama sehemu ya Kuboresha Afya.

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Brigedia Generali (Mst.) Emannuel Maganga leo ameongoza na kushiriki mazoezi ya mbio kwa umbali wa kilomita 12 zilizolenga kuhamasisha watu wapende kufanya mazoezi ya mwili ili kuimarisha Afya zao.

Mbio hizo zilizoandaliwa na Kigoma Jogging Club zimehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, watumishi kutoka Sekretarieti ya Mkoa  na Taasisi mbalimbali za Manispaa ya Kigoma Ujiji.

Katika kuhitimisha mbio hizo Brigedia Generali (Mst.) Maganga amewashukuru Uongozi wa Kigoma Jogging Club kwa kuanzisha mazoezi hayo ambayo ni muhim kwa afya “ nichukue fursa hii kuwashukuru na kuwapongeza ninyi mliofikiri kuanzisha kitu kama hiki kwani leo tulivyokimbia pamoja tumepata faida nyingi, ukiachiliambali kujenga afya tumefahamiana na kujenga umoja, hata hivyo baadhi yetu hufanya mazoezi haya kwa ratiba zao lakini tunapokuwa pamoja hivi tunatiana moyo zaidi kuliko mtu akifanya mazoezi peke yake anaweza kujisikia uvivu na kuacha”


Aidha amewaasa watumishi wote na wananchi kupenda kufanya mazoezi kama njia ya kuondokana na maradhi mbalimali mathalani shinikizo la damu. “Ninawaomba msiishie leo tu, mazoezi haya yawe endelevu kwa ajili ya faida ya afya zetu” 
Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Brigedia Generali (Mst.) Emannuel Maganga akiwa na Wakuu wa Taasisi, Idara mbalimbali wakati wa kukimbia mbio za uhamasishaji Mazoezi

Mkuu wa Mkoa wa Kgoma (mwenye fulana nyekundu) Mhe. Brigedia Generali (Mst. ) Emanuel Maganga akiongoza mazoezi ya kukimbia (kushoto kwake) ni Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mhe. Samson Anga (kulia kwake) ni Katibu Tawala Msaidizi Utawala na Rasilimali Watu Sekretarieti ya Mkoa wa Kigoma Bw. Daniel Machunda.

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Brigedia Generali (Mst.) Emannuel Maganga (Mwenye fulana ya drafti) pamoja na Katibu Tawala Msaidizi Utawala na Rasilimali Watu Sekretarieti ya Mkoa wa Kigoma Bw. Daniel Machunda. (mwenye fulana ya bluu) wakihitimisha zoezi la mbio za kuhamasisha mazoezi  kwa kuimba wimbo wa Mchakamchaka Katika Uwanja wa Michezo wa Lake Tanganyika.

Watumishi kutoka sekta mbalimbali katika Manispaa ya Kigoma Ujiji wakishiriki mbio za uhamasishaji wa Mazoezi kama sehemu ya kuboresha Afya zao.

Baadhi ya watumishi wa Taasisi mbalimbali za Serikali walioshiriki katika mbio za uhamasishaji mazoezi zilizofanyika Siku ya Jumamosi tarehe 03 Disemba, 2016 Katika Manispaa ya Kigoma Ujiji.



Picha zote na

G.D. Ng'honoli
  Afisa Habari na Mawasiliano wa Sekretarieti ya Mkoa wa Kigoma


No comments:

Post a Comment