Friday 28 March 2014

Serikali kutumia Tsh. 32 Bilioni katika mradi Mkubwa wa Maji Mkoani Kigoma

Jumla ya Tsh. 32 Bilioni zitatumika katika mradi Mkubwa wa Maji Mkoai Kigoma katika Maispaa ya Kigoma Ujiji mradi unasimamiwa na Kampuni ya Specon Ltd. , fedha hizo ikiwa ni msaada kutoka chi za jumuiya ya Ulaya pamoja na nguvu ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Hatua za kusukwa nondo za tanki la maji eneo la Mjimwema karibu na Ziwa Tanganyika
 Mradi huu utahusisha ujenzi wa matanki makubwa ya Maji yeye ujazo wa lita 2,000,000 za maji kilamoja yatakayojegwa katika maeneo tofauti dai ya maispaa ya Kigoma/Ujiji, (Mnarani na Mjimwema).
Baadhi ya Wataaalamu kutoka Ofisi ya Mamlaka ya Maji Kigoma Wakikagua maedeleo ya mradi wa maji.
 Kukamilika kwa mradi huu kutapunguza shida ya upatikanaji wa Maji katika Manispaa ya Kigoma/Ujiji kwa 95%. Aidha, sambamba na ujenzi wa matanki hayo kutakuwa na ujenzi wa matanki mengine 16 pamoja na kutandaza mabomba ya kupitishia maji urefu wa 16.6 km. .
Wafanyakazi wakiwa katika hatua ya kumwaga jamvi la moja ya matanki ya maji. Mradi huu unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Machi, 2015.


No comments:

Post a Comment