Tuesday 25 March 2014

Viongozi wa Burundi wasifia Uimarishwaji wa Ndege Mkoani Kigoma

 Mkuu wa Mkoa wa Rutana Mhe. Juvenali Ndayiragije kutoka  nchini Burundi amesifia jitihada za serika ya Tanzania katika Ujenzi na upanuzi wa Uwanja wa Ndege Mkoani Kigoma ambao kwa kiwango kikubwa umekuwa msaada kwa abiria wa Burundi kuutumia katika safari malimbali ndani na nje ya Afrika.
 Mhe. Ndayiragije amesema hayo wakati alipotembelea kiwanja cha ndege cha Mkoani Kigoma jana, ambapo alifuatana na wakuu wa wilaya, Maafisa washauri katika ngazi mbalimbali Mkoani Rutana.

Naye Meneja wa Kiwanja cha Ndege Mkoani Kigoma aliwaeleza waviongozi hao kuwa ni vema sasa wakawahimize wananchi wao kutumia uwanja wa ndege wa Kigoma ambao upo karibu.



Katibu Tawala Wa Mkoa wa Kigoma Eng. Dkt. John Ndunguru(kushoto) akiwa na baadhi ya wajumbe kutoka Mkoa wa Rutana Nchini burundi, wajumbe hao wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Rutana Juvenali Ndayiragije, pamoja na Wakuu wa Wilaya sita na Maafisa washauri wa Sekta mbalimbali Mkoani huo walifika Mkoani Kigoma kwa nia ya kutembea lakini hasa kujionea Maendeleo ya Uwanja wa ndenge wa Mkoa wa Kigoma.

Sehemu ya Uwanja wa Ndege wa Kigoma inayoonekana ni njia ya Kutua na Kurukia ndege.

No comments:

Post a Comment