Monday 28 April 2014

Mkoa wa Kigoma kuwa mwenyeji wa maadhimisho ya siku ya Uchangiaji damu Kitaifa



Mkoa wa Kigoma kuwa mwenyeji wa maadhimisho ya siku ya Uchangiaji damu Kitaifa
Mkoa wa Kigoma utakuwa mwenyeji wa maadhimisho ya siku ya uchangiaji damu Kitaifa yatakayofanyika tarehe 14 Juni, 2014 ambapo Mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho hayo atakuwa mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Salma Kikwete.
Akitoa Taarifa ya maadhimisho hayo wakati wa kikao cha hamasa kwa viongozi Katibu Tawala Msaidizi Seksheni ya Afya Dkt. Leonard Subi aliwaambia wajumbe kuwa maadhimishohayo yataanza tarehe 1 Juni, 2014 na kumalizika tarehe 14 Juni, 2014 ambayo itakuwa siku ya Kilele.
Dkt. Subi ameeleza kuwa Halmashauri na Manispaa zitakuwa na vilele vya maadhimisho hayo kadri ya ratiba itakavyopangwa.
Wananchi wanatakiwa kujitokeza kwa wingi katika tendo la kuchangia damu ili kusaidia kuokoa maisha ya kinamama wajawazito na watoto wachanga ambao wengi wao wamekuwa wakipoteza maisha kwa kukosa damu.
Naye Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserkali la Evidence for Action (E4A) Bw.Graig Ferla alisema  vifo vingi vya kinamama wajawazito vimekuwa vikitokea kabla au mara baada ya kujifungua, suala la ukosefu wa damu katika hospitali limekuwa ni kubwa.
 Alitoa wito kwa jamii kuwa na moyo wa kuchangia damu kwa hiari na kuliweka suala hili kama agenda ya kila mara katika jamii ili kunusuru vifo vya kinamama na watoto.
Katibu Tawala Seksheni ya Afya, Dkt. Leonard Subi akitoa neno la ufunguzi wakati wa kikao cha hamasa kwa viongozi wa Serikali juu ya maandalizi ya siku ya Uchangiaji damu  itakayoadhimishwa Kitaifa Mkoani Kigoma tarehe 14 Juni, 2014

Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mhe. Ramadhan Maneno akitoa hotuba ya Ufunguzi kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma siku ya Kikao cha hamasa cha maandalizi ya siku ya Uchangiaji damu kilichofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma.

Mkuu wa Wilaya ya Uvinza Bi. Hadijah Nyembo akichangia hoja wakati wa kikao cha hamasa cha maandalizi ya siku ya uchangiaji damu kilichofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma.


Bw. Graig Ferla ambaye ni Mkurugenzi wa Shirila lisilo la kiserikali la E4A linalojihusisha na masuala ya uchangiaji damu akielezea namna jamii inavyotakiwa kutambua na kuguswa na tendo la uchangiaji damu.

Katibu Tawala Seksheni ya Afya, Dkt. Leonard Subi akitoa  takwimu za vifo vya kinamama na watoto wachanga  za kila Wilaya Mkoani Kigoma ambapo Mkoa umejitahidi kupungua vifo hivyo kwa kiwango kikubwa.
 Habari na Picha- G.D. Ng'honoli (Afisa Habari wa RS)

No comments:

Post a Comment