NMB kuchangia vifaa
Tiba katika Hospitali ya maweni
Benki ya Taifa ya
Biashara NMB imesema itachangia vifaa tiba vyenye thamani ya Shilingi Milioni
kumi (10,000,000) katika Hospitali ya Rufaa ya Maweni Mkoani Kigoma.
Akizungumza wakati wa
Uzinduzi wa Tawi la Benki hiyo Meneja wa Kanda wa Benki ya NMB Bw. Ibrahim
Agustino alisema kwa kutambua mchango mkubwa na ushirikiano wa wateja na ungozi
wa Mkoa wa Kigoma Benki ya NMB imeona ni muhimu kuchangia huduma za Afya ili
wananchi waendelee kuwa na afya njema nahivyo kuendelea na Shughuli za
uzalishaji mali na kukuza kipato.
Naye Meneja wa tawi la
Benki ya NMB Mkoa wa Kigoma Bw. Rodgers Malangu alisema tendo la NMB kuchangia
katika afya ni moja ya malengo yake katika kujenga mahusiano mazuri kati ya
wateja, jamii na Serikali kwa ujumla.
Alisema kwa sasa Benki
hiyo inatarajia Kufungua matawi yake sehemu zote za Wilaya mpya hususan
Buhigwe, Uvinza na Kakonko.
Bw. Rodgers Malangu ambaye ni Meneja
wa Tawi la Benki ya NMB Mkoani Kigoma akitoa maneno ya Ukaribisho wakati wa
hafla fupi ya Uzinduzi wa Tawi la Benki hiyo Mkoani Kigoma
|
Meneja wa Kanda wa Benki ya NMB Bw.
Ibrahim Agustino akitoa hotuba wakati wa Uzinduzi wa Tawi la Benki ya NMB
Mkoani Kigoma.
|
Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mhe. Ramadhan Maneno akitoa hotuba
ya Ufunguzi wa Tawi la Benki ya NBM kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa (mgeni rasmi).
|
Meneja wa NMB tawi la Kigoma Bw.
Rodgers Malangu akitoa maelezo kwa Mgeni rasmi Mhe. Ramadhan Maneno namna Benki ya NMB inavyowahudumia wateja
wenye mahitaji mbalimbali ya kibenki.
|
No comments:
Post a Comment